Monday 20 February 2017

Mr. T Touchez amleta rasmi Harmorapa

Zikiwa zimepita wiki mbili sasa tangu rapa anayechipukia Harmorapa kukutana na producer anayefanya vyema kwa sasa kwenye sekta ya muziki Mr. T Touchez na kufanya kazi pamoja inasemekana kazi ya rapa huyo iko tayari kwenda mtaani hivi sasa.
Producer T Touchez amefunguka na kusema kazi hiyo imekamilika kila kitu na sasa ipo tayari kwenda kwa wananchi ili waweze kumsikia rapa huyo ambaye baadhi ya watu wanatilia shaka kuwa hawezi muziki, huku wengine wakimpa moyo kuwa akaze atatoka kwenye muziki na kufanikiwa kama watu wengine.
“Harmorapa final mix niambie hii nyimbo niitoe lini? “. Alihoji Mr T Touchez 
Awali Mr. T Touchez alipokutana na Harmorapa alimpa ushauri kuwa aache maneno bali anatakiwa kuleta muziki mzuri ili kuweza kukata ngebe za baadhi ya watu ambao huenda hawaamini katika uwezo wake. 
Harmorapa mpaka sasa ni kati ya wasanii wachache ambao wanachipukia na kuweza kuwa na kismati cha kupendwa na watu wa lika zote kutokana na namna anavyoishi na jinsi ambavyo yeye mwenyewe anajiweka.
Hadi sasa amefanikiwa kukutana na watu wengi maarufu akiwemo Producer nguli wa muziki wa bongo fleva P Funk Majani, Juma Nature, na Erick Shingongo ambao wote walionyesha kufurahi kukutana na kijana huyo. 
Harmorapa alipotembelea Mkurugenzi wa Global Publishers, Erick Shingongo ofisini kwake

from Blogger http://ift.tt/2lmpuYx
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2kQ9s7t

No comments:

Post a Comment