Friday 4 August 2017

TAZAMA Dunia Yetu Ilivyo Ndogo Ukilinganisha Na Sayari Zingine

Dunia yetu inaonekana ni kubwa sana ambapo ukubwa huo unatufanya sisi tujione ni wadogo sana. Ni kweli Dunia yetu ni kubwa sana ukilinganisha na sisi, lakini tukiangalia upande wa pili na tukailinganisha na sayari au vitu vingine ulimwenguni basi lazima utastaajabu kuona jinsi gani sisi na Dunia yetu tulivyowadogo sana.
Kutokana na kukua kwa teknolojia siku hadi siku wanasayansi wameweza kuziona sayari, nyota na vitu vingine vilivyokuwa mbali sana kupitia darubini kubwa zilizokuwa huko angani. Picha zifuatazo zitakuonesha ni jinsi gani Dunia yetu ilivyokuwa ndogo ukilinganisha na vitu vingine vilivyokuwa huko angani.
Hii inafahamika kama SuperCluster of Galaxies au muunganiko wa galaksi mbali mbali kitaalamu inaitwa Laniakea (Mbingu isiyopimika). Hapo mshale ulipoonyesha ndipo galaxy yetu inayoitwa Milky Way ilipo.
Hapo mshale ulipoelekeza ndipo galaksi ya Milky Way ilipo
Kama tukiikuza picha ya SuperCluster kwa ukaribu kuelekea kwenye galaxy yetu ya Milky Way hivi ndivyo itakavyoonekana kwa ukaribu. MilkyWay ndiyo galaxy yetu tulipo sisi, hapo kwenye mshale ulipoelekeza ndipo Jua letu, Dunia, pamoja na Sayari zingine zote zilizokuwa kwenye mfumo wetu wa Jua zilipo. Hivyo vidoti vyenye rangi mbali mbali vinavyong’aa ndizo nyota zote tunazoziona usiku. Hapo kati kuna shimo jeusi (Black Hole) ambalo linafyonza hizo nyota zote ikiwemo na sayari zake kuingia humo ndani. Siku moja na sisi Jua letu litafika hapo baada ya miaka bilioni kadhaa huko mbele.
Hapo mshale ulipoelekeza ndipo mfumo wetu wa jua ulipo (Jua na sayari zote ikiwamo na dunia yetu)
Jua letu limechukua asilimia 99.86% ya sehemu yote kwenye mfumo wetu wa jua (Solar System) na ni kubwa sana ambapo Dunia milioni 1.3 zinaweza kutosha ndani yake.
Hapo mshale ulipolekeza ni dunia
Pete za kwenye sayari ya Zohali ni kubwa sana ambapo Dunia sita zinaweza kutosha kwenye pete hizo. Hizi pete ni mchanganyiko wa mapande makubwa ya barafu na mawe yanayozunguka sayari hiyo ya Zohali.
Dunia sita zinaweza kutosha kwenye pete ya zohali
Hilo doti kubwa jekundu unaloliona ni kimbunga kikubwa sana kilichomo katika sayari ya Sumbula. Kimbunga hicho ni kikubwa sana ambapo Dunia tatu zinaweza tosha.
Dunia tatu zinaweza kutosha kwenye kimbunga cha kwenye sayari ya Sumbula
Hii picha ilipigwa mwaka 2013 na chombo kinachoitwa NASA Cassin Spacecraft. Hicho kidoti cha bluu kilichooneshewa mshale mwekundu ni Dunia yetu. Umbali kutoka eneo picha hii ilipopigwa mpaka Duniani ni maili milioni 898.
Hicho kidoti cha bluu kilichooneshwa na mshale ni Dunia yetu

from Blogger http://ift.tt/2v3e9Dq
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2ferV0l

No comments:

Post a Comment