Friday 4 August 2017

Facebook Wataanza Kulipa Watu Kupitia Video Wanazopakia kwenye mtandao huo

Facebook wapo mbioni kuhakikisha watu wanaanza kulipwa kwa kupakia video na maudhui mengine kwenye mtandao huo, ambapo hivi karibuni wameinunua kampuni ya masuala ya hakimiliki mtandaoni Source 3 ili kuhakikisha hakuna wizi wa maudhui yatakayokuwa yanapakiwa kwenye mtandao huo, ikiwa pamoja na kuzuia watu watakao kuwa wana nakili maudhui ya watu wengine ili kujiingizia pesa kupitia matangazo yatakayokuwa yanatokea wakati video au kitu chochote kikiwa kinatazamwa na mashabiki wa mpakiaji.
Source 3 watakuja na teknolojia ambayo inafanya kazi sawa na ile inayotumika kwenye YouTube inayofahamika kama YouTube Content ID. Teknolojia hiyo itawawezesha wapakiaji video kwenye Facebook kuweza kuzuia video zao zisipakiwe na watu wengine au kuchukua mapato yatakayopatikana kwenye video hiyo kutoka kwa mtu ambaye si mmiliki halali wa video.
Pia Facebook walizindua app maalumu kwa wamiliki wa kurasa. App hiyo itawawezesha wamiliki wa kurasa kwenye mtandao huo kuweza kuwapatia mashabiki wao machapisho ya kwenye kurasa zao moja kwa moja huku wakitengeneza pesa kupitia machapisho hayo.
Kwa sasa Facebook inazaidi ya mashabiki bilioni 2 ambao kila mwezi lazima waingie kwenye mtandao huo, Facebook inatarajiwa kuwa ndiyo sehemu kubwa ya kuingiza pesa kwa watu watakaokuwa wanamiliki kurasa kwenye mtandao huo, huku YouTube ikishika mkia.

from Blogger http://ift.tt/2wrx6xe
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2ferYJz

No comments:

Post a Comment