Friday 17 March 2017

Harmonize: Mapenzi yetu na Wolper sio ya kiki

Harmonize amefunguka kuwa ni kweli waligombana na mpenzi wake Jacqueline Wolper na haikuwa kiki kama watu wanavyofikiria.
Muimbaji huyo amekiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM Jumatano hii, kuna baadhi ya vitu vilisababisha wagombane lakini kwa sasa kila kitu kinaenda sawa.
“Kuna vitu vilitokea tukajikuta hatuko sawa, lakini Mungu ndio mwenye kheri tukawa tupo pamoja tukajua kabisa kuwa hiki kitu Jack hakipendi au mimi. Sasa hivi kila kitu kinaenda sawa na mapenzi yetu sio ya kiki, nafasi yetu kwenye jamii imefanya ionekane kuwa ni kiki,” amesema Harmo.
Hitmaker huyo wa Matatizo ameongeza kuwa alianza kuwa na mahusiano na Wolper muda mrefu tangu kipindi hana gari anatembea kwenye bajaji.

from Blogger http://ift.tt/2nyVgCC
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2mBNGGt

No comments:

Post a Comment