Thursday 26 November 2015

MREMA KUPINGA MATOKEO MAHAKAMANI


Mbunge wa Vunjo James Mbatia (kushoto) akiwa na Augustino Lyatonga Mrema bungeni 2014
Mbunge wa Vunjo James Mbatia (kushoto) akiwa na Augustino Lyatonga Mrema bungeni 2014
Aliyekuwa Mgombea Ubunge Jimbo la Vunjo Augustino Mrema amefungua kesi Mahakama Kuu Moshi, kupinga matokeo ya Uchaguzi yaliyomtangaza James Mbatia wa NCCR-Mageuzi mshindi.
Mbatia alishinda Ubunge katika jimbo hilo kwa jumla ya kura 60,187 aliyemfuata ni Innocent Shirima aliyepata kura 16,617 na Mrema alipata kura 6,416.
Mrema amemtuhumu Mbatia, Mkurugenzi wa Uchaguzi Vunjo na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kukiuka baadhi ya taratibu za uchaguzi.
Akiongea na waandishi baada ya kufungua kesi amesema, “nimeamua kufungua kesi kwa sababu nataka haki yangu.”
Ameiomba Mahakama kufuta matokeo ya Uchaguzi wa Ubunge katika Jimbo hilo na kutaka uchaguzi urudiwe.
Kwa mujibu wa Ndugu Mrema, James Mbatia alisambaza karatasi za kupigia kura kabla ya siku ya uchaguzi akitaka wananchi wampigie kura, amesema kuwa Mbatia alisambaza karatasi za kupigia kura mpaka makanisani na kwenye misikiti.
Chanzo: JF

from Blogger http://ift.tt/1T56PtR
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/1R738oP

No comments:

Post a Comment