Monday 20 March 2017

Elibariki Kingu: Kwa Hili la Makonda, Naomba Niwe wa Kwanza kufukuzwa CCM..!!!

Nilisema Nitanyamaza lakini Nimeshindwa. Nimethibitisha bila mashaka Clouds kuvamiwa na Rc akiwa na ulinzi na askari wenye silaha mpaka kwenye matangazo.
Najua hofu mliyonayo watanzania juu ya huyu Rc.
Ikiwa mamlaka zitaendelea kufumbia macho.Mimi Elibariki Immanuel Kingu mbunge wa CCM nitakuwa wa kwanza kufukuzwa CCM kama kupinga matendo maovu ya Rc huyu itaonekana ni usaliti kwa nchi.
Haiwezekani Rais wetu atukanwe kila kona kwa matendo ya mtu huyu.
Wana CCM ukimya wetu kwenye hili halikubaliki.
Magufuli juzi ametuliza Dodoma kwa kuongea kwa hisia.Idara za usalama kweli mmeamua kuacha tutukanwe?
Naomba sasa niweke kumbukumbu sawa najua mnamchafua kila anayempinga RC huyu kwa matendo yake ambayo yanakiuka utawala bora.
Naomba niwe wa kwanza kufukuzwa CCM kwa kumpinga Rc Makonda
Elibariki Immanuel Kingu

from Blogger http://ift.tt/2ncZu4Z
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2mGYbHA

No comments:

Post a Comment