Friday 2 December 2016

Biashara ya usafiri wa ndege pasua kichwa

Dar es Salaam. Wakati Serikali ikifanya jitihada kulifanya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) kushindana na kampuni binafsi, biashara ya usafiri wa anga nchini inazidi kuporomoka, ikiathiri kampuni, ajira na kipato cha huduma zinazoambatana na usafiri huo.

Wakati Air Tanzania ikiandaa wafanyakazi wapya kwa ajili ya kuhudumia ndani ya ndege mbili aina ya Bombadier zilizonunuliwa hivi karibuni, kampuni pinzani za Precision Air na Fast Jet zinapunguza wafanyakazi na safari ili kukabiliana na kuporomoka huko kwa biashara ya usafiri wa anga.

Hayo yanatokea wakati kukiwa na malalamiko ya hali ya uchumi kuwa ngumu, ikihusishwa na hatua mbalimbali ambazo Serikali ya Awamu ya Tano imekuwa ikichukua kurekebisha uchumi.

Hatua hizo za Serikali zimesababisha kudorora kwa mzunguko wa fedha na kuathiri kipato cha wananchi wengi.

from Blogger http://ift.tt/2ggrjD8
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2guGfAy

No comments:

Post a Comment