Mahakama moja nchini Sweden imemhukumu mwanasoka wa ligi daraja la pili kwenda jela miaka 2 kwa kosa la kumbaka na kumpiga mkewe.
Klabu ya Gefle imesema Bonsu amefukuzwa kwenye klabu hiyo mara moja baada ya kupatikana na hatia ya mashtaka yake.
Mchezaji huyo pia ametakiwa kulipwa kiasi cha 245,000 kronor zaidi ya million 50 za kitanzania – ikiwa ni fidia kwa mkewe, ambaye ni raia wa Sweden.
Bonsu alikutana na mkewe mnamo mwaka 2014 wakati akiitumikia klabu ya Mjolby na wakaoana mwaka uliofuatia. Miezi kadhaa baada ya ndoa alisaini kwenda klabu ya Gafle – kilomita zaidi ya 300 kutoka Mjolby.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!
from Blogger http://ift.tt/2s7oFIR
via IFTTT
from WordPress http://ift.tt/2sdS8Bp
No comments:
Post a Comment