Profesa Ibrahim Lipumba amesema aliamua kurudi CUF kwa sababu ya sintofahamu iliyokuwapo kwenye Umoja wa Katiba ya Wananchi(Ukawa) baada ya kumtangaza Edward Lowassa kuwa mgombea urais wa chama hicho.
Profesa Lipumba amesema hayo leo asubuhi wakati akihojiwa na Televisheni ya Clouds katika kipindi cha 360.
Amesema alidhani Dk Wilbroad Slaa ndiye atakuwa mgombea wa urais kwa tiketi ya Ukawa na aliafiki hilo lakini akadai hakupenda Lowassa kuwania nafasi hiyo kwa sababu ni mzigo mzito kumnadi.
from Blogger http://ift.tt/2pK9NyJ
via IFTTT
from WordPress http://ift.tt/2pAw3KP
No comments:
Post a Comment