Rais wa Brazil Michel Temer ameahama katika Ikulu ya nchi hiyo (Alvorada Palace) kwa kile alichoeleza kuwa ni kutokujisikia vizuri pamoja na kuona mizimu inayomfanya ashindwe kulala usiku.
Kiongozi huyo pamoja na mke wake, Marcela (33) wameyahama makazi hayo rasmi kwa kile walichoeleza vyombo vya habari kutokujisikia hali ya kawaida na kuona vitu vya ajabu ajabu vinavyowafanya washindwe kulala usiku na kusema huenda ikawa ni mizimu.
Rais na mkewe baada ya kuhama katika makazi hayo, wamerejea katika makazi yao ya awali (Jaburu Palace) alipokuwa akiishi wakati akiwa Makamu wa Rais chini ya uongozi wa Rais Dilma Rousseff aliyeondolewa madarakani mwaka 2016 kwa makosa ya rushwa.
Tukio hili la Rais kuhama makazi yake limekuja wakati ambao nchi hiyo ina mgogoro mkubwa wa kisiasa kufuatia tuhuma za rushwa zinazowakumba viongozi wengi wa kisiasa pamoja na taasisi za serikali.
from Blogger http://ift.tt/2nEU280
via IFTTT
from WordPress http://ift.tt/2mOaFAn
via IFTTT
from Blogger http://ift.tt/2m0NMuM
via IFTTT
from WordPress http://ift.tt/2mJCubo
via IFTTT
from Blogger http://ift.tt/2nb9DzB
via IFTTT
from WordPress http://ift.tt/2m1d1NN
via IFTTT
from Blogger http://ift.tt/2nbJQal
via IFTTT
from Blogger http://ift.tt/2mu9SBc
via IFTTT
from WordPress http://ift.tt/2mulTXn
No comments:
Post a Comment