Saturday, 21 November 2015

TAARIFA ZAIDI KUHUSU MAHUJAJI KUTOKA TANZANIA WALIOFARIKI AU KUJERUHIWA HUKO SAUDI ARABIA


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

TAARIFA ZAIDI KUHUSU MAHUJAJI KUTOKA TANZANIA WALIOFARIKI AU KUJERUHIWA HUKO SAUDI ARABIA


Mahujaji wengine wane (4) kutoka Tanzania ambao walikuwa miongoni mwa wale waliokuwa hawaonekani tangu ajali ya kukanyagana kwa mahujaji ilipotokea Makkah nchini Saudi Arabia tarehe 24 Septemba 2015 wametambuliwa kuwa, ni miongoni mwa mahujaji waliofariki  dunia. Kutambuliwa kwa mahujaji hao kunafanya idadi ya mahujaji wa Tanzania waliopoteza maisha katika ajali hiyo kufikia thelathini na mbili (32). 


Majina ya Mahujaji hao kutoka kikundi cha Khidmat Islamiya ni:-

1. Abdul Idd Hussein

2. Adam Abdul Adam

3. Rashida Adam Abdul

4. Khadija Abdukhalik Said 


Aidha, hadi sasa mahujaji saba (7) kutoka Tanzania bado hawajulikani walipo na jitihada za kuwatafuta bado zinaendelea. Majina ya Mahujaji hao ni:

1. Burhani Nziru Matata

2. Farida Khatun Abdulghani

3. Juma Jecha Jaku

4. Laila Manunga

5. Nassor Mohammed Hemed

6. Saleh Mussa Said

7. Shabinabanu Ismail Dinmohamed


Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, 

Dar es Salaam

20 Novemba, 2015

from Blogger http://ift.tt/1MttLRC
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/1QUGuQz

No comments:

Post a Comment