Kituo cha sheria na haki za binadamau LHRC kilizungumzia hatua ya tume ya taifa ya uchaguzi ya kutoweka hadharani daftari la kudumu la wapiga kura wakati huu ambapo zimebaki siku 18 tu ili watanzania waweze kupiga kura hapo oktoba 25 mwaka huu.
Wanaharakati wa haki za binadamu pia wamehoji tume ya taifa ya uchaguzi pia kuchelewa kutoa orodha ya vituo vya kupigia kura pamoja na jitihada za wadau wa uchaguzi zikiwemo asasi hizo za kiraia za kutaka kupata orodha hiyo.
Asasi za kiraia nchini Tanzania pia ziliiomba serikali kutobadilisha watendaji na makamishna wa tume ya taifa ya uchaguzi wakati huu zikiwa zimebaki siku chache kufikia tarehe ya uchaguzi mkuu ili kuondoa dhana potofu kwamba inajaribu kuweka mazingira ya kuwezesha chama tawala cha CCM kushinda uchaguzi huo.
from Blogger http://ift.tt/1j5r3Ym
via IFTTT
from WordPress http://ift.tt/1LgzOtF
No comments:
Post a Comment