Tuesday 29 September 2015

CCM haina hasara na walio hama inaumia kadi kwenda kwa watu wasio husika katika chama

KUHAMA kwa viongozi wakuu wastaafu wa serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania kutoka ndani ya chama cha mapinduzi CCM kwenda chama upinzani hakuna hasara kwa Chama hicho bali kunahasara ya kupotea kwa kazi zake kwa mtu asiye muhumu kwa chama.


Katibu wa CCM wilaya ya Njombe Mkoani Njombe, Saadi Kimati (Pichani) wakati akizungumza na waandishi huhusiana na mwenendo wa kampeni katika wilaya yake yenye majimbo matatu.


Alisema kuwa kuhama kwa Viongozi wakubwa wastaafu, Edward Lowassa mgombea urais kupitia Chasema na kuungwa mkono na umoja wa katiba ya wananchi (Ukawa), na Fredrick Sumaye waziri mkuu mstaafu sio kwa thamani kwa Chama hicho bari umuhimu wa wao kupewa kati katika chama hicho ndicho kitu cha gharama kwa chama hicho.
Katibi wa CCM wilaya ya Njombe Saadi Kimati



Alisema Chama hicho hakisikitiki kupoteza shilingi 540 ila kinasikitika kupoteza kati kwa mtu asiye na faida kwa chama hicho.




Alisema kuwa chama hicho kuondoka kwa watu hao wawili na wengine wachache walio wafuata hakuna madhara kwani chama hicho kimeongeza watu maelfu kwa maelfu kabla ya kuondoka kwa watu hao.


Kimati alisema chama chake kwa kipindi hiki cha kampeni hakina kazi ngumu ya kuwanadi wagombea wao na kuwa kinafanya kazi ya kuwakumbusha wananchi kwa kile chama kilicho chanya tangu kilipo ridhi Uhuru kutoka kwa wakoroni.

from Blogger http://ift.tt/1L1Xdif
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/1KO7tpR

No comments:

Post a Comment