Sunday 6 September 2015

Aliyekuwa kada wa Chadema Ikungi, Singida, Hamisi Mazonge, arejea CCM na kukiomba radhi


DSC01397

Aliyekuwa
katibu mwenezi CHADEMA kata ya Ikungi mkoani Singida, Hamisi Yahaya
Mazonge, akitangaza uamuzi wake wa kuhama CHADEMA na kurejea CCM,
 kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni za uchaguzi nafasi ya ubunge na
udiwani jimbo la Singida mashariki.Mazonge amedai kwamba amehama CHADEMA
baada ya kubaini chama hicho hakina sera yoyote ya kuwaletea wananchi
maendeleo.(Picha naNathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Ikungi
ALIYEKUWA
Katibu mwenezi wa CHADEMA Kata ya Ikungi wilaya ya Ikungi mkoani
Singida, Hamisi Yahaya Mazonge, amerejea CCM na kukiomba radhi Chama
chake hicho, kwa madai amekifanyia kosa kubwa wakati akiwa CHADEMA.
Mazonge
alitaja kosa hilo kuwa ni kukinyang’anya Chama cha Mapinduzi (CCM),
vijiji vya Ikungi,Ighuka, Mbwajiki na Matongo kwenye Uchaguzi wa
serikali za mitaa na kuwa chini ya mikono ya CHADEMA.
Alisema
anajutia kosa hilo la kusababisha vijiji hivyo vinne vilivyokuwa chini
ya CCM kwa miaka mingi, kuhamia CHADEMA. Amedai pia kipindi hicho
alitumia nguvu kubwa kuchangia pia vitongoji 11 kati ya vitongoji 22 vya
kata ya Ikungi,kuhamia CHADEMA.
“Wana
CCM wenzangu,kutoka chini ya sakafu ya moyo wangu,najutia sana kufanya
kosa hili ambalo kwa vyo vyote,litakuwa limeathiri kwa kiasi kikubwa
ustawi wa CCM katika kata yetu”,alisema.
Mazonge
ambaye ameonyesha dhahiri kujutia kosa hilo,amekiomba radhi Chama Cha
Mapinduzi wakati akizungumza kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni za
ubunge na udiwani katika jimbo la Singida mashariki uliofanyika katika
makao makuu ya wilaya ya Ikungi mkoani Singida.
Aidha,alisema
amefikia uamuzi wa kurejea CCM baada ya kubaini CHADEMA jimbo la
Singida mashariki kwa miaka mitano iliyopita, imedumaza kwa kiwango
kikubwa  maendeleo ya jimbo hilo.
Mazonge
ameahidi kuwa kuanzia sasa atakuwa mwanachama mwaminifu wa CCM na
atatumia nguvu za ziada, kuhakikisha vijiji na vitongoji hivyo vinarejea
mikononi mwa CCM.
Naye
Mkulima na mfugaji wa kijiji cha Ng’ogousoro Kata ya Isuna, Chapa Chapa
Elias, amesema amerejea CCM baada ya kutokufurahishwa na kitendo cha
CHADEMA,kupokea  makapi kutoka CCM na kuyauzia chama kizima kizima.
“Binafsi
kwa sasa CHADEMA chama ambacho kilianza kwa na nguvu ya upinzani ya
kweli, kimebadilika ghafla na kuwa kama choo ambacho kazi yake ni
kupokea kila aina ya taka taka. Kwa ujumla kwa sasa CHADEMA hakieleweki
kabisa”,alisema Chapa kwa masikitiko.
Kwa
upande wake Mchungaji wa Kanisa la Pentekoste kijiji cha Ikio Ponisian
Ghumpi, amehama CHADEMA kwa madai kwamba kwa sasa chama hico hakina
dhamira ya kweli ya kuwatumikia wananchi.
Kama
hiyo haitoshi,mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa (NEC) ya CCM kutoka
Rombo, Evod Mmanda, ambaye alikuwa kwenye msafara wa kampeni ya mgombea
mwenza wa urais,alitumia nafasi hiyo,kumwanika Tundu Lissu,hadharani na
kumwacha akiwa ‘mtupu’.
Mmanda
alisema anamfahamu vyema Lissu na kwamba uwezo wake wa kuongoza ni
mdogo, hivyo kuendelea kumchagua kuwa Mbunge ni sawa na kutafuta
matatizo.
“Wana
Singida Mashariki tokeni kwenye mchepuko (CHADEMA) na kusema kufanya
kosa si kosa, lakini mimi nasema mlifanya kosa kumchagua Tundu
Lissu”,alisisitiza.
Kuhusu
mgombe wa CCM Jonathan Njau,alisema;“Namfahamu Njau miaka 15, ni mtu
mwelewa na mpenda maendeleo. Tundu Lissu namfahamu tangu akiwa kidato
cha nne, ni mtu msanii na mhamasishaji wa fujo, kamwe ndugu zangu wa
Singida msifanye makosa ya kumrejesha madarakani tena”. Alisema.
Mmanda
alisema Lissu amekuwa akihamasisha wananchi wasishiriki katika shughuli
za maendeleo kama vile kuchangia miradi ya elimu na afya, jambo ambalo
limesababisha jimbo hilo, kuwa nyuma kimaendeleo.
“Wana
Ikungi mnahitaji madaktari, wahandisi na wataalamu wa kilimo na mifugo
kwa vile ninyi mnajishughulisha na mambo haya. Sasa kama mtu anakataa
kuchangia maendeleo, anataka mkose madaktari na wanasayansi ili
muendelee kuwa masikini. Hakika mtu huyu anayeitwa Tundu Lissu, si mzuri
na hapaswi kuchaguliwa kabisa,” alisema.
Aliongeza:
“Tundu Lissu hana nia ya dhati ya kuwaendeleza wana Singida mashariki.
Mfano mzuri ni kwamba watoto wake na wa mdogo wake wanasoma Zanzibar
kwenye shule ambazo zina maabara zilizokamilika”.

from Blogger http://ift.tt/1EIzLWB
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/1IRArUl

No comments:

Post a Comment