Baada ya kuitwa kuhojiwa kuhusu tuhuma za kuhusika na biashara ya dawa za kulevya, Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete ambaye ni mtoto wa Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete amesema taarifa hizo zilitingisha familia yake, lakini baba yake Jakaya Kikwete alimtia moyo.
Ridhiwani Kikwete
Ameyazungumza hayo katika mahojiano maalumu na Mwananchi Digital yaliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita.
Tofauti na watuhumiwa wengine waliohojiwa kuhusu matumizi na biashara ya dawa za kulevya, Ridhiwani hakutangazwa hadharani badala yake aliitwa kimyakimya na kuhojiwa na baadaye kuruhusiwa aendelee na shughuli zake baada ya kuonekana hana hatia.
Hata hivyo aliongeza kuwa baba yake Mhe, Kikwete hakushtushwa na badala yake alimpa nguvu ya kwenda kueleza ukweli .”Pengine aliamua kuficha hofu yake ili kunitia nguvu,” amesema Ridhiwani.
TAZAMA JAMAA HUYU ALIVYOKOSWA KOSWA NA KIFO KWA AJARI MTONI
from Blogger http://ift.tt/2nqhzga
via IFTTT
from WordPress http://ift.tt/2mXbjJJ
No comments:
Post a Comment