Monday, 21 August 2017

KILIMO CHA PARACHICHI NJOMBE

from Blogger http://ift.tt/2ihQFpI
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2vRpmaG

HII NDIYO KAULI YA SERIKALI KUHUSU WANAFUNZI KWENDA VYUO VIKUU BILA KUHITIMU KIDATO CHA SITA

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inapenda kuutarifu umma kuwa taarifa zinazosambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari
“Serikali yapiga Marufuku Kusoma Shahada bila kupita Kidato cha Sita,” tarifa hiyo siyo ya kweli na haijatolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mh. Joyce Ndalichako.Wizara inapenda kuufahamisha umma kuwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako hajatangaza popote na kuwa taarifa hiyo haina ukweli wowote.
Profesa Ndalichako yuko Mkoani Kigoma kwenye ziara ya ufuatiliaji wa Miradi ya Elimu, inayotekelezwa kwa ushirikiano wa Ofisi ya Rais TAMISEMI pamoja na Wizara yake.
Vile vile Wizara inapenda kutoa wito kwa watanzania kuacha kutumia mitandao ya kijamii vibaya kwa kuupotosha umma kwa taarifa ambazo siyo sahihi na hazina ukweli wowote.
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ina utaratibu wake wa kutoa taarifa hivyo inawaomba radhi wale wote waliopata usumbufu kutokana na kusambaa kwa taarifa hiyo.
Imetolewa na:
Mwasu Sware
Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
19 Agosti, 2017

from Blogger http://ift.tt/2vWsuAs
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2x52McU

DAR:MENO YA TEMBO YENYE KILO 376 YAKAMATWA NA SERIKALI

Waziri wa Maliasli na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe amesema serikali imefanikiwa kukamata jumla ya meno ya tembo 28 katika ghala moja lililopo Mbezi Beach jijini Dar es salaam, yenye uzito wa takribani kilo 376.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Waziri Maghembe amesema meno hayo yaliyokamatwa tarehe 13 na 14 mwezi wa nane mwaka huu yanaonekana ni ya tembo waliouawa miaka ya nyuma ikikadiriwa kuuawa miaka ya 2013 au 2014 na wahalifu hao kuyaweka majumbani mwao huku wakiendelea kutafuta masoko.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Mghembe akizungumza na waandishi wa habari wakati alipokuwa akiwaonesha jumla ya meno ya tembo 28 yakiwa na takribani kilo 376 yaliyokamatwa kwenye ghala katika eneo la Mbezi Beach hivi karibuni. Jumla ya watuhumiwa wa ujangili wapatao 6 tayari wameshakamatwa akiwemo Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa na Imam wa msikiti wa Huda wa Mbezi Beach, Aboubakar Zuberi Segumi ( Picha na Lusungu Helela- WMU)
Waziri Maghembe amesema tayari hadi hivi sasa watuhumiwa sita wa ujangili wameshakamtwa akiwemo Mohamedi Yahya Mohamed, almaarufu Mpemba, Aboubakar Zuberi Seguni mkazi wa Mbezi Beach ambaye pia ni mwenyekiti wa serikali za mtaa na imamu wa msikiti wa Huda uliopo Mbezi, Juma Saleh Jebo mkazi wa Manzese jijini Dar es salaam, Hamisi Rashid Omary mkazi wa Mbezi, Amir Bakari Shelukindo Mkazi wa Gairo Morogoro na Ahmed Shabani Bakari mkazi wa Mkuranga.
Wakati akiwataja watuhumiwa hao, Waziri Maghembe alisema vita dhidi ya ujangili ni ngumu kwa vile hata baadhi ya watu wasiotegemewa katika jamii kujihusisha nayo nao wamo, akitolea mfano wa mtuhumiwa, Bakari Zuberi Seguni mkazi wa Mbezi Beach ambaye pia ni mwenyekiti wa serikali za mtaa na imamu wa msikiti wa Huda uliopo Mbezi kuwa yeye ni mfano katika jamii kwa kuwa ni kiongozi wa kiserikali lakini pia ni mtu wa Mungu ambaye ni ngumu kufikiria ni miongoni mwa washirika wa biashara hiyo haramu.
Aliongeza kuwa, Tanzania kupitia Wizara yake inataka kufuta kabisa biashara ya meno ya tembo kama China walivyofanya licha ya kuwa uuzaji wa meno ya tembo kwa sasa mara baada ya kufuta soko la wazi imekuwa ikiendelea kwa njia ya mtandao.
Katika hatua nyingine , Waziri Maghemba alipaza sauti kwa mataifa kama vile Vietnam na Thailand kuacha kujihusisha na biashara hiyo na kuiomba jumuiya ya Kimataifa kuingilia ili tembo waendelee kuwepo kwa faida ya kizazi kijacho na badae na dunia kwa ujumla.
Aidha, Waziri Maghembe amesema Tanzania na Dunia kwa ujumla imepata pigo kubwa baada ya kutokea kwa mauaji ya Mkurugenzi wa Palm Foundation, Wayne Lotter raia wa Afrika Kusini yaliyotokea usiku wa jana Masaki jijini Dar es Salaam kwa kuwa alikuwa mstari wa mbele katika kuisaidia serikali katika vita dhidi ya Ujangili.

from Blogger http://ift.tt/2xhCLXd
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2vRonqY

MAMBO MATATU TUNAYOJIDANGANYA ZAIDI KUHUSU FURAHA NA MAFANIKIO MAISHANI

Ili uwe na maisha mazuri, ni lazima utapitia maisha magumu, yenye mabalaa na misukosuko, bila kujali neno mafanikio au ‘maisha mazuri’ kwako linamaanisha nini. Hutaweza kuishi maisha mazuri mpaka utakapopata ujasiri wa kuweza kuwa mkweli na nafsi yako. Si lazima kuwa mkweli kwa nafsi yako kwa asilimia mia moja, lakini kila unapozidi kuwa mkweli kwa nafsi yako ujue wazi kwamba unazidi kuyasogelea malengo uliyojiwekea.
Watu wenye “mafanikio ” huwa wanazungumza na nafsi zao mara kwa mara – mazungumzo yanayolenga kumnyoosha mustakabali wa maisha yao kuyaelekea malengo waliyojiwekea, na katika mazungumzo haya ya mtu na nafsi yake – wengi wanabaini uongo, na kauli zenye ukweli nusu wanazojiambia wenyewe.
Hakuna anayeweza kuotea mafanikio yanamaanisha nini kwako, lakini kama unaona umekwama kwa sasa, yawezekana kabisa ukawa unakwepa ukweli wa maisha kwa namna moja ama nyingine. Hujayaangalia maisha yako kiundani na kuanza kuihoji nafsi yako.
Zifuatazo ni baadhi ya kauli tunazojiambia ili kujiridhisha na hali tulizonazo hata kama hazituridhishi au tungetamani kuwa kwenye hali ya juu zaidi ya tuliyonayo sasa:
1. Nikipata “x” nitajisikia “y”
Ni jambo gumu sana kuamini kwamba una kila kitu unachohitaji ili kukufanya uwe mwenye maisha ya furaha na ni rahisi sana kujikuta umeingia kwenye mtego wa kufikiria kwamba mafanikio yako yanayofata yatakufanya ujisikie vizuri zaidi. Unajidanganya.
Mafanikio ni matokeo yanayokuja kwa wewe kuridhika kwakuwa unafanya shughuli unayoipenda kutoka moyoni. Mafanikio hayaendi kwa mtu anayefanya kinyume cha hayo (kwa asiyeridhika au kwa anayefanya shughuli asiyoipenda kwa dhati). Hii ni moja ya njiapanda kuu kabisa kimaisha.
Linapokuja swala la maisha yako, bila shaka unafikiria kwamba yanahitaji kurekebishwa kwakuwa kuna jambo haliendi sawa. Unadhani kwamba kuna jambo tofauti na wewe linalohitaji kurekebishwa ili ujisikie vizuri.
Mabadiliko yanatakiwa yaanzie ndani kuja nje (kwamba wewe mwenyewe ndio ubadilike kwanza ndipo uwaze kubadili mambo ya nje). Kuna baadhi ya hatua unazotakiwa kuchukua kwa kiasi kikubwa, mabadiliko yanatokea pale unapobadili mtazamo wako na nini unachohitaji uwe na furaha, ambacho si kingine bali utashi wako mwenyewe.
2. Nataka/naomba ‘x’
Sisi sote ni wabinafsi. Kila mmoja anataka mafanikio, furaha, pesa nyingi, uhuru na muda, mapenzi, afya nzuri — na kila kilicho kizuri maishani, tunakitaka. Kutaka yote haya si vibaya na haiepukiki, lakini kudhani kwamba yanatakiwa yashushwe kwako na wewe uanze kufaidi itakusababishia msongo wa mawazo hasa pale utapoyakosa.
Mara nyingine ukiulizwa swali kwanini unaona unastahili jambo fulani, unaweza kujikuta ukakwama na kushindwa kutoa jibu la kushawishi.
Unasema kwamba unastahili kupata mafanikio na utajiri — kwanini? Nini ulichofanya kinachokupa uhakika kwamba unastahili mafanikio na utajiri huo? Umefanya kazi kwa muda gani kuhakikisha lengo hilo linatimia? Umeyafanyia kazi malengo hayo?
Unadhani kwamba unastahili uhusiano mzuri na wenye utulivu — kwanini? Unaishi vipi na watu wengine? Ni kwa kiasi gani umeweka juhudi kuhakikisha tabia na mienendo yako inaweza kukubalika na watu wa aina unayopenda kuanzisha uhusiano nao badala ya kutaka watu wengine waendane na matakwa na tabia zako?
Haiwezekani kwenda benki kutoa pesa kabla ya kwanza kufungua akaunti na kuweka pesa zako kwenye akaunti hiyo – huu ndio utaratibu wa kimaisha. Huwezi kutarajia kupokea faida tu kama wewe mwenyewe hukufanya uwekezaji kabla. Utakapojua ukweli juu ya hili hutapata tabu unapokosa kitu. Usipoujua ukweli huu au kuamua kuudharau, basi kila mara utaona unaonewa au kutaka kila mtu awe anakutimizia mahitaji yako wewe tu.
3. Mpaka nilipofikia sasa, hakuna ninachoweza kufanya tena
Kuna wengine wanaweza kuona kwamba wamechelewa sana kufanya maamuzi katika ujana wao mpaka walipofikia sasa wanajiona wamechelewa. “Kwa sasa nina miaka 50, sio kijana kama wewe. Ningekuwa na nguvu ningeweza kufanya hayo unayosema, sasa hivi umri umeshakwenda sana.” Kauli kama hizi tumeshazisikia sana na ni kauli zenye uzito.
Lakini kuna mambo mawili yanasahauliwa au watu wenye umri kama huu wanashindwa kuyazingatia. Kwanza ni kwamba inaonesha kuwa tayari wameshakata tamaa kwenye maisha yao. Kana kwamba kufikisha miaka 50 ni sawa na kuvuka mstari wa mwisho kwenye mbio za marathon, kila kitu kinatakiwa kufikia tamati na kuanza kuhuzunika juu ya fursa ambazo ulishindwa kuzitumia maishani.
Pili ni watu wa umri huu kushindwa kujiuliza swali la msingi sana, kwa sasa nina miaka 50 – vipi ikiwa nitajaliwa umri mrefu na kuishi miaka 40 zaidi, maisha yangu yatakuwaje? Labda ukiona kwamba yawezekana ukawa na muda wa kuishi zaidi ndio utajua kwamba inabidi uweke mipango thabiti na kuanza kuitekeleza – bila kujali umechelewa kiasi gani.

from Blogger http://ift.tt/2iiC6Ca
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2x5c1d5

MAGHOROFA YA LUGUMI KUPIGWA MNADA NA SERIKALI

Kampuni ya Udalali ya Yono imetangaza kupiga mnada majengo matatu ya ghorofa yanayomilikiwa na Kampuni ya Lugumi Enterprises Limited baada ya mmiliki wake kushindwa kulipa kodi anayodaiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Agosti 20 mwaka huu katika gazeti la Sunday News lilitolewa tangazo la mnada wa majengo hayo ambayo ni mali ya Lugumi yanayotarajiwa kupigwa mnada Septemba 9 mwaka huu. Ghorofa moja lipo eneo la Upanga na kwa mujibu wa tangazo hilo, jengo hilo linafaa kwa ofisi na makazi, na majengo mawili ya Mbweni JKT yanafaa kwa makazi.
Scholastica Christian Kevela ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Yono alisema kuwa miezi minne iliyopita nyuma walifungia mali za Lugumi wakimtaka alipe malimbikizo ya kodi aliyokuwa akidaiwa, lakini hadi sasa hajafanya hivyo.
Kiongozi huyo wa Kampuni ya Udalali ya Yono ambayo ni wakala wa serikali wa kukusanya kodi kwa wadiwa sugu ambapo hushirikiana na TRA alisema mdaiwa huyo hajalipa mabilioni ya kodi anayodaiwa na hivyo wao wamepewa amri halali ya kuzipiga mnada nyumba hizo wananzozishikilia.
Kevela alikataa kutaja kiwango cha fedha ambacho Lugumi anadaiwa na TRA akabaki akisisitiza kwamba ni mabilioni ya shilingi na kwamba TRA ndio wanajua kiwango halisi. Hata hivyo hakutangaza thamani ya majengo hayo akisema kwamba, kila mtanzania aje na fedha aliyonayo kwani wao kama madalali hawana kiwango maalum.
Aidha, Kevela aliwataka wananchi kulipa kodi bila shuruti kuepuka nyumba zao kupigwa mnada huku akisema kwamba wasipofanya hivyo na deni lao likafika kwa Yono, wao watafanya kazi yao kiukamilifu.

from Blogger http://ift.tt/2v5vAkj
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2vS8eS5

Saturday, 12 August 2017

MAZAO MATANO YANAYOINGIZIA SERIKALI FEDHA ZA KIGENI ZAIDI

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imeamua kufufua mazao matano ambayo yanaingiza kwa wingi fedha za kigeni nchini.
Amesema mbali ya korosho, Serikali imeamua kuboresha mazao ya tumbaku, chai, kahawa na pamba.
Ametoa kauli hiyo kwa nyakati tofauti jana na leo wakati akiwahutubia wananchi kwenye maeneo mbalimbali akiwa katika ziara ya kikazi ya siku nne mkoani Tabora.
Alisema kuanzania sasa serikali imepiga marufuku matumizi ya dola za Marekani kwenye ununuzi wa zao la tumbaku kwa sababu mazao mengine makuu hapa nchini yananunuliwa kwa fedha za Kitanzania.
“Ni kwa nini tumbaku inunuliwe kwa dola za Marekani ilhali mazao mengine yananunuliwa kwa fedha za Tanzania? Korosho, pamba, chai na kahawa wakulima wetu kote huko wanalipwa kwa fedha za Tanzania, kwa nini tumbaku iwe tofauti?” alihoji.
Alisema wenye makampuni wanaweza kukaa kwenye vikao vyao na kupanga bei zao kwa dola za Marekani lakini pindi wanapoingia nchini, watalazimika kufanya malipo kwa kutumia fedha ya Tanzania kwani mfumo malipo kupitia dola za Marekani umekuwa ukiwaibia wakulima kwa muda mrefu.
Waziri Mkuu amewataka watendaji na watumishi wa Halmashauri na wilaya za mkoa wa Tabora wasimamie zao la tumbaku ili kuinua kilimo cha zao hilo na kuwanufaisha wakulima.
“Maafisa kilimo na maafisa ushirika mnapaswa kulisimamia zao hili na siyo kuwaachia maafisa wa makampuni yanayonunua tumbaku.” 
“Kwa muda mrefu mlizembea na kuwaachia maafisa wa makampuni ya ununuzi ndiyo washughulike na wakulima. Nataka mbadilike, kuweni karibu na wakulima na muwasaidie kulima kisasa na kwa kutumia pembejeo,” alisema.
“Wasaidieni wakulima watoke kwenye mfumo wa kukopa pembejeo, wahimizeni wajiwekee akiba ili msimu ukianza wawe na fedha ya kununua pembejeo. Wakulima wanalaliwa sababu ya mikopo ya pembejeo. Makato yanakuwa mengi kiasi kwamba mkulima ahambulii chochote,” alisema.
Waziri Mkuu anaendelea na ziara yake wilayani Kaliua ambako atazungumza na wananchi.
IMETOLEWA NA: 
OFISI YA WAZIRI MKUU, 
IJUMAA, AGOSTI 11, 2017.

from Blogger http://ift.tt/2w0kws1
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2uQlz9C

Thursday, 10 August 2017

RAIS MAGUFULI AKUTANA NA TAJIRI NAMBA MOJA DUNIA

Taasisi ya Bill and Mellinda Gates imetenga Dola za Marekani Milioni 350 sawa na takribani Shilingi Bilioni 777.084 za Tanzania kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali katika sekta ya kilimo, afya na mifumo ya kielektroniki ya upatikanaji wa taarifa.
Mwenyekiti Mwenza wa taasisi hiyo Bw. Bill Gates amesema hayo leo tarehe 10 Agosti, 2017 Ikulu Jijini Dar es Salaam muda mfupi baada ya kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.
Bw. Bill Gates amesema kama ambavyo taasisi yake imeshirikiana na Tanzania kwa kiasi kikubwa katika kuimarisha huduma za afya hapa nchini, fedha hizo zitaelekezwa katika utekelezaji wa miradi zaidi ya afya ikiwemo kupunguza vifo vya uzazi, kukabiliana na ugonjwa wa malaria, kuimarisha lishe na kukabiliana na utapiamlo, zitaelekezwa katika sekta ya kilimo ambako zitasaidia kuongeza uzalishaji wa mazao, kuzalisha mbegu bora na kuboresha ufugaji utakaoongeza chakula na pia zitasaidia kuweka mifumo ya kisasa ya upatikanaji wa taarifa.
Bw. Bill Gates ameelezea kufurahishwa na maendeleo ya uchumi wa Tanzania pamoja na uongozi na msimamo wa Rais Magufuli juu ya kutaka miradi hiyo ilete matokeo yenye manufaa, na amesema atakuja Tanzania mara nyingi ili kuimarisha zaidi ushirikiano na kufuatilia utekelezaji wa miradi.
Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli amemshukuru Bw. Bill Gates kwa mchango mkubwa unaotolewa na taasisi ya Bill and Mellinda Gates katika miradi mbalimbali hapa nchini ikiwemo fedha ambazo taasisi hiyo itazitoa katika kipindi cha miaka mitano kuanzia sasa na amemhakikishia kuwa Serikali yake itahakikisha fedha hizo zinaleta matokeo yaliyokusudiwa.
Mazungumzo kati ya Mhe. Rais Magufuli na Bw. Bill Gates yamehudhuriwa na Waziri wa Kilimo, Ufugaji na uvuvi Dkt. Charles Tizeba na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu.
Wakati huo huo, Mhe. Magufuli amekutana na kufanya Mazungumzo na Kaimu Balozi wa Marekani hapa nchini Mhe. Dkt. Inmi Patterson ambaye amesema Marekani itatoa fedha za nyongeza kiasi cha Dola Milioni 225 sawa na Shilingi Bilioni 499.500 za Tanzania katika mwaka ujao kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo itakayogusa sekta za elimu, afya, lishe bora, utawala bora.
Mhe. Inmi Patterson amesema Marekani imeongeza fedha hizo katika miradi inayotekelezwa hapa nchini kwa sababu ina dhamira ya dhati ya kushirikiana na Tanzania na itahakikisha uhusiano na ushirikiano huu unaendelezwa na kukuzwa zaidi.
Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli amemshukuru Mhe. Balozi Inmi Patterson kwa mchango mkubwa ambao Marekani imekuwa ikiutoa kwa Tanzania na amemhakiki kuwa Serikali ya Awamu ya Tano itaendeleza na kukuza zaidi ushirikiano wake na Marekani, na pia amemuomba awahimize wafanyabiashara na wawekezaji wengi zaidi wa Marekani waje kuwekeza na kufanya biashara hapa nchini kutokana na fursa lukuki zilizopo.
Mhe. Rais Magufuli pia ameiomba Marekani kusaidia kujenga hospitali kubwa ya kitaifa katika makao makuu ya nchi Mkoani Dodoma ili kuongeza uwezo wa Mkoa huo kutoa huduma za matibabu ikilinganishwa na ilivyo hizi sasa.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
10 Agosti, 2017

from Blogger http://ift.tt/2vSW1h6
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2uu1BlR