Wednesday, 23 August 2017

SHULE 18 ZAFUNGIWA NA SERIKALI KIGAMBONI

Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni imeendesha zoezi la kufunga shule za msingi na awali ambazo hazina usajili katika manispaa hiyo.
Zoezi hilo limesimamiwa na Kaimu Afisa Elimu wa Manispaa ya Kigamboni, Mwalimu Mathew Komba pamoja na Wakaguzi wa Elimu katika manispaa hiyo.
Image result for WANAFUNZI
Katika zoezi la ukaguzi katika shule mbalimbali, mapungufu mbalimbali yalipatikana ambayo ni pamoja na shule kutokuwa na usajili,
madarasa machache, kutokuwa na vyoo kwa ajili ya wanafunzi na walimu ambapo baadhi ya shule zinatumia vyoo vya misikiti au wanafunzi kujisaidia kwenye vyoo vya jirani .
Katika siku ya kwanza ya ukaguzi huo, timu hiyo imezifunga shule 18 kati ya 58 zilizobainishwa kutokuwa na usajili katika kata za Kigamboni, Vijibweni na Tungu.
Kati ya shule zilizofungwa ni Malaika Nursery School, Kigamboni English Medium School, Patmos, Montecarlos, Riziki, Taqwa, Firdaus na Meck.
Aidha, uongozi wa Manispaa ya Kigamboni imewataka wazazi kutowapeleka watoto wao kwenye shule hizo mpaka hapo watakapokimilisha taratibu walizowekewa pamoja na kupata usajili.

from Blogger http://ift.tt/2wyc0Bq
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2wyv6Yd

AMRI YA SERIKALI KWA WAMILIKI WOTE WA MAGAZETI

from Blogger http://ift.tt/2g59mwi
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2xsRZsK

UKITAKA KUSTAAFU MAPEMA ZINGATIA MAMBO HAYA.

  • Watu wengi sana wanatamani kuwa na uwezo na uhakika wa kustaafu mapema, lakini ni wachache sana wanachukua hatua mahususi kuhakikisha wanalitimiza jambo hilo.
  • Ili uweze kustaafu mapema, mambo matatu yanahitajika: kipato cha uhakika, kuweka akiba na kuwekeza akiba yako.
  • Jambo la kuzingatia ili utimize lengo hili ni kufanya mambo hayo matatu yawe ndio kipaumbele chako maishani.
  • Vijana wanajulikana kwa kuwa na tabia ya kutopenda kufata sheria, na linapokuja swala la matumizi ya pesa zao wanazozipata kwa jasho lao – wengi zaidi huwa hawataki hata ushauri kabisa.

    Lakini uwezekano wa kustaafu mapema unaweza kuwafanya wengi washawishike kuachana na ubishi wao na kufikiria uhakika wa maisha yao ya uzeeni na kuanza kuchukua hatua za uhakika kuyanyoosha wangali bado vijana na wenye nguvu za kufanya kazi.

    Image result for GRAND PARENTS

    Zifuatazo ni njia hizo na jinsi ya kufanya:

    1. Tengeneza chanzo imara cha mapato
    Kama huna chanzo cha mapato, hutakuwa na nafasi hata ya kuanza kujenga utajiri. Hatua ya kwanza kabisa ya kuhakikisha unapata uhuru wa kipato ni kuwa na chanzo cha uhakika cha kipato ili uwe na uhakika kwamba kutokana na kipato hicho, unaweza kuweka akiba pamoja na kuwekeza kwa ajili ya maisha ya baadaye.

    Kwa baadhi ya watu, hii yaweza kumaanisha ufanye kazi kwa ufanisi kwenye ajira yako ya sasa ili uweze kutimiza lengo hili. Ukiwa na chanzo cha uhakika cha mapato, hata ikiwa ni kutokana na kazi za mkataba au tenda za kulipwa kwa siku, bado unaweza kuweka mipango ya baadaye na kuanza kuitekeleza, japo kidogo kidogo.

    2. Weka akiba sehemu kubwa ya kipato hicho
    Ukishakuwa na kipato cha uhakika, jambo muhimu ni kuhakikisha kuwa hutumii pesa yote unayopata. Kujifunza jinsi ya kuishi maisha ya gharama nafuu chini ya kipato chako ni muhimu ili uweze kubaki na pesa (hasa ukianzia ujanani mwako) na uweze kujiwekea akiba itakayokusaidia kwa maisha yako yote yaliyobaki.

    kwanza, miongoni mwa njia rahisi zaidi za kuhakikisha utakuwa na fedha uzeeni mwako ni kujiunga na mfuko wa hifadhi za kijamii. Mifuko hii itakusaidia kutoa michango yako kila mwisho wa mwezi au kwa muda maalum na kuja kuipata utakapotimiza umri wako wa kustaafu. Kwa waajiriwa, michango hii huwa inakatwa moja kwa moja kutoka kwenye mshahara wako – kwahiyo huna haja ya kuwa na wasiwasi kuhusu hilo – lakini kwa ambao hawajaajiriwa, unaweza kujiunga kwenye mifuko hii kama mtu binafsi, kwakuwa inaruhusiwa kufanya hivyo pia. Michango unayoiweka ni kiasi kidogo sana cha pesa kwa mwezi, lakini faida yake uzeeni ni kubwa.

    Pia, unaweza kupunguza matumizi yako ya pesa kwa kupunguza gharama za nyumba (kama umepanga) ili kodi yako kwa mwezi isizidi asilimia 30 ya kipato chako.

    3. Wekeza akiba yako kwenye vitega uchumi vitakavyoongezeka au kutopungua thamani
    Kuwa na pesa nyingi kwenye akiba yako ni jambo zuri, lakini unapoiwekeza pesa hiyo yaweza kusababisha tofauti kubwa sana kwenye safari yako ya kustaafu mapema.

    Kuna wanaoamua kuwekeza kwenye sekta ya majumba, na inaweza ukunufaisha kwakuwa una uwezekano wa kuingiza kipato cha kila mwezi kutokana na kodi za pango.

    Kwa wale wasiovutiwa na biashara ya majumba, unaweza kujifunza na kuwekeza kwa kununua hisa za makampuni mbalimbali ambayo yana rekodi nzuri ya ukuaji.

    Mwanzo wa safari ya mafanikio ya kuwa na uhuru wa kipato unaanza kwa uamuzi wako kwamba kufanya hivyo ni muhimu sana kwako. Kisha ukiwa unazingatia malengo yako, basi unaweza kutimiza kila unachokitaka bila wasiwasi.

from Blogger http://ift.tt/2vYuBW9
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2wyags4

ULIPAJI KODI YA ARDHI KWA SIMU ZA MKONONI WAANZISHWA NA SERIKALI

Ili kujua unadaiwa kiasi gani cha kodi ya pango la ardhi kwa kutumia simu ya mkononi bonyeza *152*00# au kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi yaani SMS halafu unatuma kwenda namba 15200 na baada hapo unaweza kulipia kwa njia ya Mpesa, Tigo Pesa au kulipia tawi lolote la benki ya NMB na CRDB.
Image result for i phone
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ikishirikiana na Wizara ya Fedha, imesambaza maafisa wake katika Halmashauri 169 kote nchini kutoa mafunzo katika vituo vyote vya makusanyo ya kodi ya ardhi na tozo nyingine kwa kutumia simu ya mkononi ili kuondoa kabisa mfumo wa zamani wa malipo.
Zaidi ya maafisa 170 kutoka makao makuu ya Wizara ya Ardhi, Wizara ya Fedha na kutoka kanda nane za ardhi wameanza kutoa elimu hiyo katika Halmashauri na vituo vyote vya makusanyo ya kodi ya ardhi ili kurahisisha ulipaji kodi ya ardhi kwa wananchi kwa kutumia simu zao na kuondoa usumbufu.
Mfumo wa ulipaji kodi ya pango la ardhi kwa njia ya simu ya mkononi ni mfumo wa kielektroniki wa Government electronic Payment Gateway (GePG) katika makusanyo ya kodi ya pango la ardhi ambao utamrahisishia wananchi kulipia popote walipo kwa kutumia simu zao kwa urahisi zaidi.
Mwananchi yeyote anayemiliki kiwanja au shamba lililopimwa na kupatiwa hati, ataweza kutumia simu yake ya mkononi kujua kiasi cha kodi ya pango la ardhi anachodaiwa na kulipa kwa kutumia simu yake ya mkononi.
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeanza rasmi kutumia mfumo huu wa kielektroniki wa GePG katika makusanyo ya kodi ya pango la ardhi pamoja na tozo nyingine zinazotokana na sekta ya ardhi nchini na kuondoa kabisa mfumo wa zamani.
Mfumo huu utamrahisishia mwananchi kulipa kodi ya pango la ardhi popote alipo, ikiwa ni pamoja na kulipia tozo nyingine mbalimbali za sekta ya ardhi. Mmiliki wa kipande cha ardhi ataweza kujua anadaiwa kiasi gani cha kodi ya pango la ardhi na kulipia popote alipo bila kusumbuka kufuata huduma hizo katika vituo vya makusanyo.
Kwa majaribio ya ukusanyaji kodi ya pango la ardhi kwa kutumia mfumo wa kielektroniki yalifanywa katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani na baada ya mafanikio makubwa kuonekana elimu ikatolewa kwa watendaji wote wa sekta ya ardhi katika Halmashauri zote za mkoa wa Dar es salaam kabla ya zoezi hilo kuhamishiwa mikoani.
Kwa zile huduma nyingine za sekta ya ardhi ambazo zinahusisha malipo kama vile upekuzi katika daftari la msajili (official search), mwananchi atapaswa kutembelea ofisi za Wizara ya ardhi zilizo katika eneo lake na kupatiwa makadirio ya kulipia huduma husika pamoja na namba ya malipo itakayomuwezesha kulipia aidha kwa njia ya benki au simu ya mkononi.
Kwa sasa kikosi kazi kinachotoa mafunzo juu ya matumizi ya mfumo huu kimeshaanza kuelemisha mikoa mingine baada ya kupata mafanikio mazuri katika mkoa wa Dar es Salaam. Lengo kubwa la kutumia mfumo huu ni kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa maduhuli ya serikali pamoja na kurahisisha ulipaji kodi ya pango la ardhi nchini.

from Blogger http://ift.tt/2xsNb6q
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2xspM4Y

MAABARA YA NYUKLIA YAANZA KUJENGWA NASERIKALI

Serikali imetenga shilingi bilioni 2.3 kwa ajili ya ujenzi wa maabara ya kisasa ya nyuklia katika Tume ya Nguvu za Atomiki (TAEC). Lengo la maabara hiyo ni kutoa huduma bora za kisasa za masuala ya mionzi kwa nchi za Afrika.
Aidha, vifaa vyenye thamani ya shilingi bilioni 11.5 kwa ajili ya maabara hiyo vilivyotolewa na Umoja wa Ulaya (EU) vimeanza kuwasili nchini na kuhifadhiwa kwenye maabara za tume hiyo.
Akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa maabara hiyo jana, Waziri wa Elimu, Sayansi, na teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako alisema shilingi bilioni 2.3 hizo zimetolewa na Serikali na zimetokana na fedha za ndani.
Alisema Serikali imetoa kwanza shilingi bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa jengo hilo linalotarajiwa kukamilika Februari mwakani. Kiasi kilichobaki cha shilingi bilioni 1.3 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo kitafuatia ili maabara hiyo ya kisasa iweze kutumiwa na watu mbalimbali nchini na Afrika nzima.
“Tunamshukuru Rais John Magufuli kwa kuwezesha,” alisema Profesa Ndalichako. “Maendeleo ya nchi yanasongwa hasa katika kuhakikisha tume hii inapata maendeleo na kuchangia fedha katika mfuko huu wa Serikali.”
Akizungumza katika hafla hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAEC, Brigedia Jenerali Fulgence Msafiri, alisema maabara hiyo itatoa huduma mbalimbali za matumizi salama ya mionzi pamoja na kuwa msaada kwa wanafunzi wa vyuo vikuu katika ngazi ya shahada ya Uzamili na uzamivu.
HT @ Nipashe

from Blogger http://ift.tt/2wnr704
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2wygo3t

MAMLAKA YA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA YAVUNJWA NA RAIS MAGUFULI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 23 Agosti, 2017 amemteua Luteni Kanali Frederick Felix Milanzi kuwa Kamishna wa Operesheni wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya.
Luteni Kanali Frederick Felix Milanzi anachukua nafasi ya Bw. Mihayo Msikela ambaye amerejeshwa Makao Makuu ya Polisi.
Uteuzi wa Luteni Kanali Frederick Felix Milanzi unaanza mara moja.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amezungumza na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa Kulevya Bw. Rogers William Siyanga ambaye amemhakikishia kuwa kazi ya kukabiliana na tatizo la biashara na matumizi ya dawa za kulevya inaendelea vizuri.

Bw. Rogers William Siyanga amesema tatizo la dawa za kulevya lilikuwa kubwa na ametaja dawa za kulevya ambazo Mamlaka inapambana nazo kuwa ni bangi, heroine, cocaine, kemikali bashirifu na kwamba kwa sasa imeanza kukamata na kuharibu mashamba ya bangi na bangi iliyovunwa.

Amebainisha mikakati mitatu inayotumika katika mapambano dhidi ya tatizo hilo kuwa ni kuzuia dawa za kulevya zisiingie nchini, kutoa elimu kuanzia shule za msingi, sekondari, vyuo na kwenye jamii ili watu waache kutumia dawa za kulevya na kutoa tiba kwa watu walioathirika na dawa za kulevya, na pia ametoa wito kwa watu wenye waathirika wa dawa za kulevya kuwapeleka katika mamlaka hiyo ili watibiwe.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

23 Agosti, 2017

from Blogger http://ift.tt/2ipaI5F
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2xsSeE9

Monday, 21 August 2017

KISA CHA NDEGE NDOGO (DRONE) ILIYOPELEKEA MZEE WA GHANA KUHIJI MAKA

Share this
Mzee Al-Hassan Abdullah ni mzee masikini anayeishi kijijini nchini Ghana. Hadithi yake ilisambaa sana kwenye mitandao ya kijamii nchini Uturuki baada ya mzee huyo kuwauliza wafanyakazi wa kituo cha runinga cha nchini Uturuki waliokuwa wakirekodi kipindi nchini Ghana iwapo ndege ndogo isiyokuwa na rubani (drone) iliyokuwa inatumiwa na wafanyakazi hao kurekodi “kama ndege hiyo inaweza kumpeleka Makka kuhiji” amesafirishwa kwenda Mji huo Mtakatifu kwa imani ya Uislam kwa gharama za Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki na michango iliyotolewa na raia mbalimbali nchini Uturuki walioguswa na alichokisema Mzee Abdullah.
Kilichotokea ni kwamba ndege hiyo ilidondoka karibu kabisa na nyumba ya Mzee Abdullah wakati waandishi hao wanarekodi kipindi maalum. Mzee huyu baada ya kuiona ndege hiyo aliiokota na kumsubiri rubani wake aliyekuwa anaifata aichukue. Akiwa anamkabidhi rubani ndege hiyo, ndipo Mzee Abdullah akamuuliza iwapo wana ndege nyingine kubwa zaidi ya hiyo inayoweza kumpeleka mpaka Makka ili akatimize ibada ya kuhiji kama walivyo mamilioni ya waumini wengine watakaohiji mwaka huu. Rubani huyo aliamua kupimga picha mzee huyu na kuandika maneno aliyoulizwa kisha kuituma kwenye akaunti zake za mitandao ya kijamii. Ujumbe huu ulisambaa mara moja na kuwagusa wengi kiasi cha Serikali ya nchi hiyo kuamua kulipia safari yake. Wananchi walioguswa pia waliweza kutoa mchango wao kama sadaka kumuwezesha kwenda kutimiza ibada hiyo.
Ujumbe wake uliposambaa sana kwenye mitandao ya kijamii nchini Uturuki, Waziri wa Nchi za Nje, Mevlüt Çavuşoğlu aliguswa na kushughulikia safari ya mzee Abdullah ambaye ni masikini wa kutupwa kwenda Makka. Mzee Abdullah aliwasili jijini Istanbul, Uturuki juzi Ijumaa akitokea Accra, Ghana na alipokewa na Shirika la Misaada nchini Uturuki ambalo limelenga kusaidi nchi ya Ghana.
Mzee Al-Hassan Abdullah: Kushoto alipokuwa anamkabidhi rubani ndege ndogo baada ya kuanguka karibu na nyumba yake Kulia ni katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa Istanbul, Uturuki
Abdullah aliliambia Shirika la Utangazaji la Anadolu la jijini Ankara, Uturuki kuwa amefurahi kuwa jijini Istanbul na kwamba ni Mungu ndiye aliyembariki kuweza kupata msaada kutoka Serikali ya Uturuki. “Namshukuru Mungu na namuombea kila aliyenisaidia kutimiza ndoto yangu. Msaada wa Serikali ya uturuki ni wa muhimu sana kwangu na ninaamini utakuwa ni uthibitisho wa urafiki kati ya mataifa yetu na kuonesha udugu kwa waislam,” alisema.
Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya misaada iliyompokea mzee huyu, Cihad Gökdemir amesema kwamba ujumbe wa Mzee Abdullah ulisambaa zaidi kwenye vyombo vyote vya habari nchini humo baada ya mfanyakazi wa kituo hicho cha runinga kuweka picha ya mzee huyo kupitia mtandao wa Twitter. “Hapo ndipo watu wengi walipoanza kuwasiliana na mfanyakazi huyo awaongoze jinsi ya kumsaidia Mzee Abdullah, watu wote – wafanyabiashara hadi makampuni. Mwisho, Ofisa wa Polisi kutoka Ubalozi wa Uturuki nchini Ghana akawasiliana naye. Anawashukuru sana watu wa Uturuki,” alisema Gökdemir.

from Blogger http://ift.tt/2xkhXhI
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2x5wrmr

KILIMO CHA PARACHICHI NJOMBE

from Blogger http://ift.tt/2ihQFpI
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2vRpmaG

HII NDIYO KAULI YA SERIKALI KUHUSU WANAFUNZI KWENDA VYUO VIKUU BILA KUHITIMU KIDATO CHA SITA

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inapenda kuutarifu umma kuwa taarifa zinazosambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari
“Serikali yapiga Marufuku Kusoma Shahada bila kupita Kidato cha Sita,” tarifa hiyo siyo ya kweli na haijatolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mh. Joyce Ndalichako.Wizara inapenda kuufahamisha umma kuwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako hajatangaza popote na kuwa taarifa hiyo haina ukweli wowote.
Profesa Ndalichako yuko Mkoani Kigoma kwenye ziara ya ufuatiliaji wa Miradi ya Elimu, inayotekelezwa kwa ushirikiano wa Ofisi ya Rais TAMISEMI pamoja na Wizara yake.
Vile vile Wizara inapenda kutoa wito kwa watanzania kuacha kutumia mitandao ya kijamii vibaya kwa kuupotosha umma kwa taarifa ambazo siyo sahihi na hazina ukweli wowote.
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ina utaratibu wake wa kutoa taarifa hivyo inawaomba radhi wale wote waliopata usumbufu kutokana na kusambaa kwa taarifa hiyo.
Imetolewa na:
Mwasu Sware
Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
19 Agosti, 2017

from Blogger http://ift.tt/2vWsuAs
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2x52McU

DAR:MENO YA TEMBO YENYE KILO 376 YAKAMATWA NA SERIKALI

Waziri wa Maliasli na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe amesema serikali imefanikiwa kukamata jumla ya meno ya tembo 28 katika ghala moja lililopo Mbezi Beach jijini Dar es salaam, yenye uzito wa takribani kilo 376.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Waziri Maghembe amesema meno hayo yaliyokamatwa tarehe 13 na 14 mwezi wa nane mwaka huu yanaonekana ni ya tembo waliouawa miaka ya nyuma ikikadiriwa kuuawa miaka ya 2013 au 2014 na wahalifu hao kuyaweka majumbani mwao huku wakiendelea kutafuta masoko.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Mghembe akizungumza na waandishi wa habari wakati alipokuwa akiwaonesha jumla ya meno ya tembo 28 yakiwa na takribani kilo 376 yaliyokamatwa kwenye ghala katika eneo la Mbezi Beach hivi karibuni. Jumla ya watuhumiwa wa ujangili wapatao 6 tayari wameshakamatwa akiwemo Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa na Imam wa msikiti wa Huda wa Mbezi Beach, Aboubakar Zuberi Segumi ( Picha na Lusungu Helela- WMU)
Waziri Maghembe amesema tayari hadi hivi sasa watuhumiwa sita wa ujangili wameshakamtwa akiwemo Mohamedi Yahya Mohamed, almaarufu Mpemba, Aboubakar Zuberi Seguni mkazi wa Mbezi Beach ambaye pia ni mwenyekiti wa serikali za mtaa na imamu wa msikiti wa Huda uliopo Mbezi, Juma Saleh Jebo mkazi wa Manzese jijini Dar es salaam, Hamisi Rashid Omary mkazi wa Mbezi, Amir Bakari Shelukindo Mkazi wa Gairo Morogoro na Ahmed Shabani Bakari mkazi wa Mkuranga.
Wakati akiwataja watuhumiwa hao, Waziri Maghembe alisema vita dhidi ya ujangili ni ngumu kwa vile hata baadhi ya watu wasiotegemewa katika jamii kujihusisha nayo nao wamo, akitolea mfano wa mtuhumiwa, Bakari Zuberi Seguni mkazi wa Mbezi Beach ambaye pia ni mwenyekiti wa serikali za mtaa na imamu wa msikiti wa Huda uliopo Mbezi kuwa yeye ni mfano katika jamii kwa kuwa ni kiongozi wa kiserikali lakini pia ni mtu wa Mungu ambaye ni ngumu kufikiria ni miongoni mwa washirika wa biashara hiyo haramu.
Aliongeza kuwa, Tanzania kupitia Wizara yake inataka kufuta kabisa biashara ya meno ya tembo kama China walivyofanya licha ya kuwa uuzaji wa meno ya tembo kwa sasa mara baada ya kufuta soko la wazi imekuwa ikiendelea kwa njia ya mtandao.
Katika hatua nyingine , Waziri Maghemba alipaza sauti kwa mataifa kama vile Vietnam na Thailand kuacha kujihusisha na biashara hiyo na kuiomba jumuiya ya Kimataifa kuingilia ili tembo waendelee kuwepo kwa faida ya kizazi kijacho na badae na dunia kwa ujumla.
Aidha, Waziri Maghembe amesema Tanzania na Dunia kwa ujumla imepata pigo kubwa baada ya kutokea kwa mauaji ya Mkurugenzi wa Palm Foundation, Wayne Lotter raia wa Afrika Kusini yaliyotokea usiku wa jana Masaki jijini Dar es Salaam kwa kuwa alikuwa mstari wa mbele katika kuisaidia serikali katika vita dhidi ya Ujangili.

from Blogger http://ift.tt/2xhCLXd
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2vRonqY

MAMBO MATATU TUNAYOJIDANGANYA ZAIDI KUHUSU FURAHA NA MAFANIKIO MAISHANI

Ili uwe na maisha mazuri, ni lazima utapitia maisha magumu, yenye mabalaa na misukosuko, bila kujali neno mafanikio au ‘maisha mazuri’ kwako linamaanisha nini. Hutaweza kuishi maisha mazuri mpaka utakapopata ujasiri wa kuweza kuwa mkweli na nafsi yako. Si lazima kuwa mkweli kwa nafsi yako kwa asilimia mia moja, lakini kila unapozidi kuwa mkweli kwa nafsi yako ujue wazi kwamba unazidi kuyasogelea malengo uliyojiwekea.
Watu wenye “mafanikio ” huwa wanazungumza na nafsi zao mara kwa mara – mazungumzo yanayolenga kumnyoosha mustakabali wa maisha yao kuyaelekea malengo waliyojiwekea, na katika mazungumzo haya ya mtu na nafsi yake – wengi wanabaini uongo, na kauli zenye ukweli nusu wanazojiambia wenyewe.
Hakuna anayeweza kuotea mafanikio yanamaanisha nini kwako, lakini kama unaona umekwama kwa sasa, yawezekana kabisa ukawa unakwepa ukweli wa maisha kwa namna moja ama nyingine. Hujayaangalia maisha yako kiundani na kuanza kuihoji nafsi yako.
Zifuatazo ni baadhi ya kauli tunazojiambia ili kujiridhisha na hali tulizonazo hata kama hazituridhishi au tungetamani kuwa kwenye hali ya juu zaidi ya tuliyonayo sasa:
1. Nikipata “x” nitajisikia “y”
Ni jambo gumu sana kuamini kwamba una kila kitu unachohitaji ili kukufanya uwe mwenye maisha ya furaha na ni rahisi sana kujikuta umeingia kwenye mtego wa kufikiria kwamba mafanikio yako yanayofata yatakufanya ujisikie vizuri zaidi. Unajidanganya.
Mafanikio ni matokeo yanayokuja kwa wewe kuridhika kwakuwa unafanya shughuli unayoipenda kutoka moyoni. Mafanikio hayaendi kwa mtu anayefanya kinyume cha hayo (kwa asiyeridhika au kwa anayefanya shughuli asiyoipenda kwa dhati). Hii ni moja ya njiapanda kuu kabisa kimaisha.
Linapokuja swala la maisha yako, bila shaka unafikiria kwamba yanahitaji kurekebishwa kwakuwa kuna jambo haliendi sawa. Unadhani kwamba kuna jambo tofauti na wewe linalohitaji kurekebishwa ili ujisikie vizuri.
Mabadiliko yanatakiwa yaanzie ndani kuja nje (kwamba wewe mwenyewe ndio ubadilike kwanza ndipo uwaze kubadili mambo ya nje). Kuna baadhi ya hatua unazotakiwa kuchukua kwa kiasi kikubwa, mabadiliko yanatokea pale unapobadili mtazamo wako na nini unachohitaji uwe na furaha, ambacho si kingine bali utashi wako mwenyewe.
2. Nataka/naomba ‘x’
Sisi sote ni wabinafsi. Kila mmoja anataka mafanikio, furaha, pesa nyingi, uhuru na muda, mapenzi, afya nzuri — na kila kilicho kizuri maishani, tunakitaka. Kutaka yote haya si vibaya na haiepukiki, lakini kudhani kwamba yanatakiwa yashushwe kwako na wewe uanze kufaidi itakusababishia msongo wa mawazo hasa pale utapoyakosa.
Mara nyingine ukiulizwa swali kwanini unaona unastahili jambo fulani, unaweza kujikuta ukakwama na kushindwa kutoa jibu la kushawishi.
Unasema kwamba unastahili kupata mafanikio na utajiri — kwanini? Nini ulichofanya kinachokupa uhakika kwamba unastahili mafanikio na utajiri huo? Umefanya kazi kwa muda gani kuhakikisha lengo hilo linatimia? Umeyafanyia kazi malengo hayo?
Unadhani kwamba unastahili uhusiano mzuri na wenye utulivu — kwanini? Unaishi vipi na watu wengine? Ni kwa kiasi gani umeweka juhudi kuhakikisha tabia na mienendo yako inaweza kukubalika na watu wa aina unayopenda kuanzisha uhusiano nao badala ya kutaka watu wengine waendane na matakwa na tabia zako?
Haiwezekani kwenda benki kutoa pesa kabla ya kwanza kufungua akaunti na kuweka pesa zako kwenye akaunti hiyo – huu ndio utaratibu wa kimaisha. Huwezi kutarajia kupokea faida tu kama wewe mwenyewe hukufanya uwekezaji kabla. Utakapojua ukweli juu ya hili hutapata tabu unapokosa kitu. Usipoujua ukweli huu au kuamua kuudharau, basi kila mara utaona unaonewa au kutaka kila mtu awe anakutimizia mahitaji yako wewe tu.
3. Mpaka nilipofikia sasa, hakuna ninachoweza kufanya tena
Kuna wengine wanaweza kuona kwamba wamechelewa sana kufanya maamuzi katika ujana wao mpaka walipofikia sasa wanajiona wamechelewa. “Kwa sasa nina miaka 50, sio kijana kama wewe. Ningekuwa na nguvu ningeweza kufanya hayo unayosema, sasa hivi umri umeshakwenda sana.” Kauli kama hizi tumeshazisikia sana na ni kauli zenye uzito.
Lakini kuna mambo mawili yanasahauliwa au watu wenye umri kama huu wanashindwa kuyazingatia. Kwanza ni kwamba inaonesha kuwa tayari wameshakata tamaa kwenye maisha yao. Kana kwamba kufikisha miaka 50 ni sawa na kuvuka mstari wa mwisho kwenye mbio za marathon, kila kitu kinatakiwa kufikia tamati na kuanza kuhuzunika juu ya fursa ambazo ulishindwa kuzitumia maishani.
Pili ni watu wa umri huu kushindwa kujiuliza swali la msingi sana, kwa sasa nina miaka 50 – vipi ikiwa nitajaliwa umri mrefu na kuishi miaka 40 zaidi, maisha yangu yatakuwaje? Labda ukiona kwamba yawezekana ukawa na muda wa kuishi zaidi ndio utajua kwamba inabidi uweke mipango thabiti na kuanza kuitekeleza – bila kujali umechelewa kiasi gani.

from Blogger http://ift.tt/2iiC6Ca
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2x5c1d5

MAGHOROFA YA LUGUMI KUPIGWA MNADA NA SERIKALI

Kampuni ya Udalali ya Yono imetangaza kupiga mnada majengo matatu ya ghorofa yanayomilikiwa na Kampuni ya Lugumi Enterprises Limited baada ya mmiliki wake kushindwa kulipa kodi anayodaiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Agosti 20 mwaka huu katika gazeti la Sunday News lilitolewa tangazo la mnada wa majengo hayo ambayo ni mali ya Lugumi yanayotarajiwa kupigwa mnada Septemba 9 mwaka huu. Ghorofa moja lipo eneo la Upanga na kwa mujibu wa tangazo hilo, jengo hilo linafaa kwa ofisi na makazi, na majengo mawili ya Mbweni JKT yanafaa kwa makazi.
Scholastica Christian Kevela ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Yono alisema kuwa miezi minne iliyopita nyuma walifungia mali za Lugumi wakimtaka alipe malimbikizo ya kodi aliyokuwa akidaiwa, lakini hadi sasa hajafanya hivyo.
Kiongozi huyo wa Kampuni ya Udalali ya Yono ambayo ni wakala wa serikali wa kukusanya kodi kwa wadiwa sugu ambapo hushirikiana na TRA alisema mdaiwa huyo hajalipa mabilioni ya kodi anayodaiwa na hivyo wao wamepewa amri halali ya kuzipiga mnada nyumba hizo wananzozishikilia.
Kevela alikataa kutaja kiwango cha fedha ambacho Lugumi anadaiwa na TRA akabaki akisisitiza kwamba ni mabilioni ya shilingi na kwamba TRA ndio wanajua kiwango halisi. Hata hivyo hakutangaza thamani ya majengo hayo akisema kwamba, kila mtanzania aje na fedha aliyonayo kwani wao kama madalali hawana kiwango maalum.
Aidha, Kevela aliwataka wananchi kulipa kodi bila shuruti kuepuka nyumba zao kupigwa mnada huku akisema kwamba wasipofanya hivyo na deni lao likafika kwa Yono, wao watafanya kazi yao kiukamilifu.

from Blogger http://ift.tt/2v5vAkj
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2vS8eS5

Saturday, 12 August 2017

MAZAO MATANO YANAYOINGIZIA SERIKALI FEDHA ZA KIGENI ZAIDI

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imeamua kufufua mazao matano ambayo yanaingiza kwa wingi fedha za kigeni nchini.
Amesema mbali ya korosho, Serikali imeamua kuboresha mazao ya tumbaku, chai, kahawa na pamba.
Ametoa kauli hiyo kwa nyakati tofauti jana na leo wakati akiwahutubia wananchi kwenye maeneo mbalimbali akiwa katika ziara ya kikazi ya siku nne mkoani Tabora.
Alisema kuanzania sasa serikali imepiga marufuku matumizi ya dola za Marekani kwenye ununuzi wa zao la tumbaku kwa sababu mazao mengine makuu hapa nchini yananunuliwa kwa fedha za Kitanzania.
“Ni kwa nini tumbaku inunuliwe kwa dola za Marekani ilhali mazao mengine yananunuliwa kwa fedha za Tanzania? Korosho, pamba, chai na kahawa wakulima wetu kote huko wanalipwa kwa fedha za Tanzania, kwa nini tumbaku iwe tofauti?” alihoji.
Alisema wenye makampuni wanaweza kukaa kwenye vikao vyao na kupanga bei zao kwa dola za Marekani lakini pindi wanapoingia nchini, watalazimika kufanya malipo kwa kutumia fedha ya Tanzania kwani mfumo malipo kupitia dola za Marekani umekuwa ukiwaibia wakulima kwa muda mrefu.
Waziri Mkuu amewataka watendaji na watumishi wa Halmashauri na wilaya za mkoa wa Tabora wasimamie zao la tumbaku ili kuinua kilimo cha zao hilo na kuwanufaisha wakulima.
“Maafisa kilimo na maafisa ushirika mnapaswa kulisimamia zao hili na siyo kuwaachia maafisa wa makampuni yanayonunua tumbaku.” 
“Kwa muda mrefu mlizembea na kuwaachia maafisa wa makampuni ya ununuzi ndiyo washughulike na wakulima. Nataka mbadilike, kuweni karibu na wakulima na muwasaidie kulima kisasa na kwa kutumia pembejeo,” alisema.
“Wasaidieni wakulima watoke kwenye mfumo wa kukopa pembejeo, wahimizeni wajiwekee akiba ili msimu ukianza wawe na fedha ya kununua pembejeo. Wakulima wanalaliwa sababu ya mikopo ya pembejeo. Makato yanakuwa mengi kiasi kwamba mkulima ahambulii chochote,” alisema.
Waziri Mkuu anaendelea na ziara yake wilayani Kaliua ambako atazungumza na wananchi.
IMETOLEWA NA: 
OFISI YA WAZIRI MKUU, 
IJUMAA, AGOSTI 11, 2017.

from Blogger http://ift.tt/2w0kws1
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2uQlz9C

Thursday, 10 August 2017

RAIS MAGUFULI AKUTANA NA TAJIRI NAMBA MOJA DUNIA

Taasisi ya Bill and Mellinda Gates imetenga Dola za Marekani Milioni 350 sawa na takribani Shilingi Bilioni 777.084 za Tanzania kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali katika sekta ya kilimo, afya na mifumo ya kielektroniki ya upatikanaji wa taarifa.
Mwenyekiti Mwenza wa taasisi hiyo Bw. Bill Gates amesema hayo leo tarehe 10 Agosti, 2017 Ikulu Jijini Dar es Salaam muda mfupi baada ya kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.
Bw. Bill Gates amesema kama ambavyo taasisi yake imeshirikiana na Tanzania kwa kiasi kikubwa katika kuimarisha huduma za afya hapa nchini, fedha hizo zitaelekezwa katika utekelezaji wa miradi zaidi ya afya ikiwemo kupunguza vifo vya uzazi, kukabiliana na ugonjwa wa malaria, kuimarisha lishe na kukabiliana na utapiamlo, zitaelekezwa katika sekta ya kilimo ambako zitasaidia kuongeza uzalishaji wa mazao, kuzalisha mbegu bora na kuboresha ufugaji utakaoongeza chakula na pia zitasaidia kuweka mifumo ya kisasa ya upatikanaji wa taarifa.
Bw. Bill Gates ameelezea kufurahishwa na maendeleo ya uchumi wa Tanzania pamoja na uongozi na msimamo wa Rais Magufuli juu ya kutaka miradi hiyo ilete matokeo yenye manufaa, na amesema atakuja Tanzania mara nyingi ili kuimarisha zaidi ushirikiano na kufuatilia utekelezaji wa miradi.
Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli amemshukuru Bw. Bill Gates kwa mchango mkubwa unaotolewa na taasisi ya Bill and Mellinda Gates katika miradi mbalimbali hapa nchini ikiwemo fedha ambazo taasisi hiyo itazitoa katika kipindi cha miaka mitano kuanzia sasa na amemhakikishia kuwa Serikali yake itahakikisha fedha hizo zinaleta matokeo yaliyokusudiwa.
Mazungumzo kati ya Mhe. Rais Magufuli na Bw. Bill Gates yamehudhuriwa na Waziri wa Kilimo, Ufugaji na uvuvi Dkt. Charles Tizeba na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu.
Wakati huo huo, Mhe. Magufuli amekutana na kufanya Mazungumzo na Kaimu Balozi wa Marekani hapa nchini Mhe. Dkt. Inmi Patterson ambaye amesema Marekani itatoa fedha za nyongeza kiasi cha Dola Milioni 225 sawa na Shilingi Bilioni 499.500 za Tanzania katika mwaka ujao kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo itakayogusa sekta za elimu, afya, lishe bora, utawala bora.
Mhe. Inmi Patterson amesema Marekani imeongeza fedha hizo katika miradi inayotekelezwa hapa nchini kwa sababu ina dhamira ya dhati ya kushirikiana na Tanzania na itahakikisha uhusiano na ushirikiano huu unaendelezwa na kukuzwa zaidi.
Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli amemshukuru Mhe. Balozi Inmi Patterson kwa mchango mkubwa ambao Marekani imekuwa ikiutoa kwa Tanzania na amemhakiki kuwa Serikali ya Awamu ya Tano itaendeleza na kukuza zaidi ushirikiano wake na Marekani, na pia amemuomba awahimize wafanyabiashara na wawekezaji wengi zaidi wa Marekani waje kuwekeza na kufanya biashara hapa nchini kutokana na fursa lukuki zilizopo.
Mhe. Rais Magufuli pia ameiomba Marekani kusaidia kujenga hospitali kubwa ya kitaifa katika makao makuu ya nchi Mkoani Dodoma ili kuongeza uwezo wa Mkoa huo kutoa huduma za matibabu ikilinganishwa na ilivyo hizi sasa.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
10 Agosti, 2017

from Blogger http://ift.tt/2vSW1h6
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2uu1BlR

MAJINA 7 YA WAHALIFU WALIOHUSIKA NA MAUAJI YA ASKARI 8 WILAYANI KIBITI

Tarehe 09.08.2017 majira ya saa 21:00 Hrs (saa tatu  usiku) katika mapori ya kijiji cha Rungungu mtuhumiwa akiambatana na Askari Polisi alikwenda kuonyesha Ngome ya watuhumiwa wenzake aliokuwa anashirikiana nao kufanya uhalifu.
Baada ya kukaribia eneo la tukio ulitokea upinzani mkali wa majibizano ya risasi jambo lililopelekea hata Abdallah Abdallah Mbindimbi @Abajani kujeruhiwa na risasi sehemu mbalimbali za mwili wake.
Kufuatia majibizano hayo, Askari Polisi walifanikiwa kuwajeruhi wahalifu 12 (kumi na mbili. Jitihada zilifanyika kuwapeleka Hospitali majeruhi wote 13 (kumi na tatu) ingawa baadae walifariki dunia kwa nyakati tofauti wakipelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kutokana na kuvuja damu nyingi zilizosababishwa na majereha ya risasi sehemu mbalimbali za miili yao. Miili ya marehemu imehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam.
Ndugu Wanahabari
Watuhumiwa 7 (Saba) kati ya 13 (kumi na tatu) waliopoteza maisha  kutokana na majibizano ya risasi wametambuliwa kuwa ni:
  1. Hassani Ali Njame
  2. Abdallah Abdallah Mbindimbi @ Abajani
  3. Saidi Abdallah Kilindo
  4. Abdulshakuru Mohamed Ubuguyu
  5. Issa Mohamed Mseketu @Mtawa
  6. Rajabu Thomas @Roja
  7. Mohamed Ally Kadude @Upolo
Miili 6 (sita) iliyobaki haikuweza kutambulika mara moja hivyo utambuzi utaendelea huko ilikohifadhiwa Hospitalini Dar es Salaam.
Ndugu Wanahabari
Vielelezo mbalimbali vilipatikana katika eneo la tukio, kama ifuatavyo:
S/N KIELELEZO UTAMBUZI
SILAHA, RISASI NA MABOMU
1. SMG = 5 Mali ya Jeshi la Polisi tukio la kupora Silaha Askari huko Mtengeni – Jaribu Mpakani
2. Anti Riot Gun 38mm = 2 Mali ya Jeshi la Polisi tukio la kupora Silaha Askari huko Mtengeni – Jaribu Mpakani
3. SAR = 1 Mali ya Jeshi la Polisi tukio la kupora Silaha Askari Polisi huko Stakishari Jijini Dar es Salaam
4. MAGAZINI = 2 Mali ya Jeshi la Polisi tukio la kupora Silaha Askari huko Mtengeni – Jaribu Mpakani
5. Risasi za SMG 158 Mali ya Jeshi la Polisi tukio la kupora Silaha Askari huko Mtengeni – Jaribu Mpakani
6. Bomu la kurusha kwa mkono = 1 Uchunguzi dhidi ya Bomu hilo unaendelea
7. Mabomu ya kutuliza ghasia = 4 Mali ya Jeshi la Polisi tukio la kupora Silaha Askari huko Mtengeni – Jaribu Mpakani
VIELELEZO VINGINE
8. Pikipiki  = 2 Pikipiki hizi zilitumika kuwasafirisha wahalifu hawa kwenye utekelezaji wa matukio ya uhalifu maeneo mbalimbali
9. Vitenge na Nguo mbalimbali Vitenge na nguo mbalimbali viliporwa baada ya kufanya tukio la kumuua Diwani wa Zamani wa Kibwiwi
10. Begi = 1 Liliporwa baada ya kumuua Mtendaji wa Kijiji cha Mangwe
Ndugu Wanahabari
Kwa mujibu wa taarifa za utambuzi wa vielelezo vilivyopatikana eneo la tukio na utambuzi wa baadhi ya miili ya watuhumiwa waliofariki  inaonyesha kuwa walishiriki matukio ya uhalifu maeneo mbalimbali kama ifuatavyo:
  1. Kuua OC CID na Watumishi 2 (Wawili) wa Idara ya Maliasili katika tukio la Jaribu Mpakani – Wilaya Kibiti
  2. Kuua Askari Polisi 8 (Nane) katika tukio la Mkengeni – Wilayani Kibiti
  3. Kuua Trafiki 2 (Wawili) katika tukio la Bungu “B” – Wilaya ya Kibiti
  4. Kumuua Diwani wa Zamani CCM katika tukio la  Kibwibwi – Wilaya ya  Kibiti
  5. Kuua Afisa Mtendaji,  Mwenyekiti wa Mtaa na Mkulima katika tukio la Kijiji cha Mangwi – Wilaya ya Kibiti
Ndugu Wanahabari
Wito wangu kwa Wananchi ni kuhusu mambo muhimu yafuatayo:
  1. Wananchi wote nchini kuondoa hofu ya kwamba eneo hili si salama. Nawaomba wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi na kwa kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha nawaomba wananchi kutoa taarifa mara moja kwa Jeshi la Polisi  wanapohisi kuna jambo lolote wanalolitilia mashaka.
  2. Natoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Pwani, hususani maeneo ya Mkuranga, Kibiti na Ikwiriri, kuendelea na shughuli zao mbalimbali za kujiletea maendeleo. Nawasihi kwa dhati kabisa waendelee kutupatia taarifa zitakazosaidia kumaliza kabisa uhalifu kwenye eneo hili. Nitumie fursa hii kuwashukuru sana wananchi wa maeneo ya Mkuranga, Kibiti na Ikwiriri kwa ushirikiano mnaotupatia ambao umesaidia sana kuwadhibiti wahalifu.
  3. Mamlaka za Hospitali, Zahanati, Vituo vya Afya, Maabara za Afya ya Binadamu na Maduka ya Kuuza Dawa za kutibu Binadamu zijiepushe na utaratibu wa kutoa matibabu kienyeji au kificho kwa watu waliojeruhiwa bila kufuata taratibu za kisheria ikiwemo kupata taarifa ya Polisi “kupitia Fomu maalum ya kuruhusu matibabu (maarufu kama PF. 3)”. Wahalifu wakijeruhiwa ni lazima watafute matibabu.
Kwa hiyo idara hizi ni muhimu sana kutoa ushirikiano ili kutuwezesha kuwakamata watuhumiwa maana baadhi yao wamekutwa na majeraha sehemu mbalimbali za miili yao na walikuwa wanaendelea kujitibia kwa kificho kwa kutumia dawa za hospitali.
Natoa wito kwa Mamlaka hizo kutoa taarifa mara moja kwa Jeshi la Polisi wanapoona ama kumbaini mtu ambaye ataonekana kuwa na majeraha na anatafuta tiba bila ya kufuata taratibu.
Ndugu Wanahabari
Napenda kuujulisha Umma kwamba wapo baadhi ya Watuhumiwa, Wafadhili na Washirika wa Uhalifu na Wahalifu wa ujambazi maeneo haya ambao bado hawajakamatwa. Jambo la kufurahisha ni kwamba taarifa zao zipo kwa Jeshi la Polisi nchini na zinaendelea kufanyiwa kazi ili  waweze kukamatwa na kufikishwa kwenye mkono wa Sheria mara moja.
Natoa wito kwa wananchi ambao wanawafahamu watuhumiwa wafuatao kutoa taarifa katika kituo chochote cha Polisi ili waweze kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.
Picha za watuhumiwa hao zitasambazwa kote nchini ili iwe rahisi kuwabaini. Majina ya watuhumiwa hao ni:
i.Anafi Rashid Kapelo @ Abuu Mariam
  1. Hassan Haruna Kyakalewa @ Abuu Salma @ Shujaa @ Dokta
iii.  Haji Ulatule
  1. Shekhe Hassan Nasri Mzuzuri
  2. Rashid Mtutula
Ndugu Wanahabari
Nimalizie kwa kusema kwamba uhalifu kwenye eneo hili ni suala la muda mfupi. Na tunaendelea vizuri sana. Hali ya usalama imeimarika sana eneo hili. Nazidi kutoa wito kwa wananchi kuendelea kuliunga mkono Jeshi la Polisi ili kufikia malengo yake ya kuzuia, kubambana na kutanzua uhalifu nchini.
 
Imetolewa na;
Simon Nyakoro Sirro
Inspekta Jenerali wa Polisi
IKWIRIRI
10.08.2017

from Blogger http://ift.tt/2useYXE
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2utQDN5

Friday, 4 August 2017

MASKINI…Mwanamke Aolewa Saa 10 Jioni, Afariki Saa 7 Usiku na Kichanga Tumboni…..

DAR ES SALAAM: Hii inauma sana! Wakati wengi wakitamani kuingia kwenye ndoa ili kuyafurahia maisha hayo, kwa binti Zai Mkiwa, mkazi wa Mtoni Kijichi jijini hapa, imekuwa tofauti kwani amejikuta akiyaonja maisha ya ndoa kwa saa chache na kisha kufariki, Amani linakudadavulia habari hii ya kusikitisha.
TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini kilichohudhuria msiba wa binti huyo, Zai ambaye alidaiwa kuwa na ujauzito mchanga, alionekana ni mwenye siha njema hadi siku ya harusi, Jumapili iliyopita (Julai 30, mwaka huu) kabla ya kukutwa na umauti usiku wa saa 7 siku hiyo.
“Yaani marehemu alikuwa na afya njema kabisa, na siku ya harusi yake hakuonesha hata dalili zozote za kuumwa japo kuna wakati alisema anahisi kama kuishiwa nguvu.
FULL KUTABASAMU
“Muda mwingi alikuwa akitabasamu, alifurahia ndoa yake kwelikweli kama unavyojua watoto wa kike wanavyofurahia siku hiyo muhimu katika maisha yao,” kilisema chanzo hicho.
NDOA ILIFUNGWA SINZA MAPAMBANO
Kikizidi kufunguka chanzo hicho kilieleza kuwa, siku ya tukio, mumewe aliyefahamika kwa jina moja la Yasin, alifika nyumbani kwa babu wa marehemu, Mzee Msafiri anayeishi Sinza Mapambano jijini hapa na kukamilisha taratibu zote za ndoa na baada ya zoezi hilo kukamilika, Zai aliambatana na mumewe kwenda nyumbani kwao, Mtoni Kijichi.
…Hali ilivyokuwa siku ya harusi yake.
“Huwezi amini kumbe ni kama alikuwa anatuaga vile, maana tumesherehekea pale kwa nderemo na vifijo, wakaondoka zao na mumewe lakini ilipofika saa 7 usiku, tunaambiwa amefariki dunia,” kilisema chanzo hicho.
ALIANZA KUTAPIKA
Chanzo hicho kilieleza kuwa, ndugu wa karibu na marehemu walipopewa taarifa za msiba huo, walielezwa kuwa Zai alipofika nyumbani kwa mumewe, saa chache kabla ya kukata roho, alianza kutapika na mumewe akamkimbiza Hospitali ya Mbagala Zakhem lakini bahati mbaya, alifariki.
“Walifika salama salmini, wakahifadhi zawadi mbalimbali walizokuwa wamepewa na kisha kulala. Ilipofika saa saba usiku nasikia ndiyo akaanza kutapika na mumewe alipoona hali inazidi kuwa mbaya akalazimika kumkimbiza hospitalini, lakini alipofikishwa tu akafariki akiwa mikononi mwa madaktari,” kilisema chanzo hicho.
MSIBA WAWEKWA ALIPOOLEWA
Chanzo hicho kiliendelea kuweka bayana kuwa, asubuhi ya Jumatatu, Julai 31, mwaka huu, ndugu walikusanyika nyumbani kwa babu wa marehemu, Sinza-Mapambano ambapo taratibu zote za msiba ikiwemo mazishi zilifanyika pale.
“Palepale tuliposherekea harusi ndipo tulipokusanyika tena kwa ajili ya msiba. Yaani lile turubai lililotumika katika sherehe ya harusi yake ndilo hilohilo lililotumika wakati wa msiba wake, inauma sana! Tukaomboleza pale na baadaye mida kama ya saa 10 jioni, mwili wa Zai ulienda kuzikwa katika Makaburi ya Sinza,” chanzo kilizidi kueleza.
NI NDANI YA MASAA 24 TU!
Ukweli ni kwamba, mambo yote hayo yametokea harakaharaka mno, ni ndani ya saa 24 tu! Kila kitu kwenye maisha ya binti huyo kikabaki kuwa historia ya majonzi na masikitiko kwa ndugu na jamaa waliobaki duniani.
MUMEWE ABAKI NA MACHUNGU
Kwa mujibu wa chanzo hicho kilisema kikiwa makaburini hapo, mume wa marehemu alionekana kama mtu aliyepigwa na bumbuwazi, haamini kwa kilichotokea, hajielewielewi kwani hata kuzungumzia undani wa mazingira ya kifo cha mkewe hakuweza.
KABLA YA NDOA ALIUMWA
Inasemekana, siku chache kabla Zai hajaolewa, aliishiwa nguvu na kukimbizwa hospitali lakini alitibiwa na kurejea nyumbani na hata ilipofika siku ya harusi, alikuwa mzima wa afya.
BABA AZUNGUMZA
Gazeti la Amani lilifanikiwa kuzungumza na baba wa marehemu, Ketel Madua ambaye alisema amepokea kwa masikitiko makubwa kwa kuondokewa na binti yake huyo, saa chache baada ya kumuoezesha. Gazeti hili linatoa pole kwa ndugu na jamaa kwa msiba wa Zai.

from Blogger http://ift.tt/2v3iC9e
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2voPqu3