Saturday 18 February 2017

TID: Nisingejiingiza Kwenye Kutumia Dawa za Kulevya Ningekuwa Tajiri Sana

Khalid Mohamed aka TID Mnyama, amekiri kuwa kujihusisha kwenye utumiaji wa dawa za kulevya kumemrudisha nyuma kiuchumi.

Akiongea kwenye kipindi cha XXL, kupitia Clouds FM Ijumaa hii, Mnyama ambaye alikiri hadharani kuwa mmoja wa mastaa walioathirika na matumizi ya dawa hizo, alisema hadi sasa angekuwa na utajiri wa kushangaza. Anasema dawa hizo zina gharama kubwa.

“Nadhani ningekuwa nimenunua kama magari mengine manane, ningekuwa nimefanya video za muziki kadhaa zenye kiwango kikubwa. Lakini nilitumia hela nyingi sana hasa pale ninapoenda kujirusha ningetumia hela nyingi sana,” alisema TID.

“Lakini hii imefikia mwishoni,” alisisitiza.

Staa huyo amedai kuwa dawa zilimfanya awe na mtazamo tofauti katika vitu vingi ambavyo alivichukulia rahisi rahisi.

“When you are high you think you are on top, nobody can touch you sababu you are under influence unaanza kugombana na watu, ukawajibu watu vibaya, but when you are clean unaweza ukafanya vitu, you can save a lot of money, you can be a better person, you can even marry a good girl, you can fall in love,” amesema Mnyama ambaye amejitolea kuwa balozi wa vita dhidi ya matumizi ya dawa za kulevya.



“It’s over now.”

Kwenye show hiyo TID aliachia wimbo mwingine uitwao Woman ambao amedai kuwa remix yake atamshirikisha Diamond.

from Blogger http://ift.tt/2m6TWoI
via IFTTT




from WordPress http://ift.tt/2kyQJSE

No comments:

Post a Comment